Saturday 11 May 2024

RAFIKI SDO YAKUTANISHA WATOTO WA BARAZA LA NGOKOLO, WATOA MAAMUZI KUJADILI CHANGAMOTO SHULENI... NGOKOLO SEKONDARI KUNA MWALIMU MMOJA TU WA SAYANSI


Na Kadama Malunde -  Malunde 1 blog

Shirika la Rafiki SDO limekutanisha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya kutengeneza Kadi alama na mpango kazi wa utekelezaji wa Mradi wa Kukuza Asasi za Kiraia (MKUA) ambapo watoto wamewasilisha changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo shuleni.

Kikao hicho kimefanyika leo Jumamosi Mei 11,2024 katika ukumbi wa ofisi ya Shirika la Rafiki SDO uliopo kata Kitangili Manispaa ya Shinyanga ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Zamda Shaban.

Meneja Mradi wa Kukuza Asasi za Kiraia (MKUA) , Maria Maduhu kutoka Shirika la Rafiki SDO amesema lengo la kikao hicho ni kutengeneza kadi alama (Viashiria na changamoto wanazopitia watoto) na kutengeneza mpango kazi wa kutatua changamoto zilizobainika katika shule nne ambazo ni shule ya Msingi Mapinduzi A na B, shule ya msingi Mwadui na Shule ya Sekondari Ngokolo zilizopo katika Manispaa ya Shinyanga.

Ameeleza kuwa kikao hicho ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Kukuza Asasi za Kiraia (MKUA) ambapo kwa Rafiki SDO unalenga kuimarisha mabaraza ya watoto ili kutetea haki zao na kujua wajibu wao na kwamba Rafiki SDO itafanya ufuatiliaji wa mpango kazi uliotengenezwa ambapo watoa maamuzi watafanya utekelezaji wa kutatua changamoto zilizojitokeza.

“Rafiki SDO inatekeleza mradi wa MKUA katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, Shinyanga na Manispaa ya Kahama. Huu ni mradi wa miaka mitatu 2022-2024”,ameongeza.

Kikao hicho kimekutanisha Watoto wa baraza la watoto la Ngokolo na Watoa Maamuzi ngazi ya kata ya Ngokolo na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.

Miongoni mwa viashiria na changamoto wanazokabiliana nazo watoto shuleni ni pamoja na uhaba wa vifaa vya kusomea na kujifunzia ikiwemo vitabu ambapo wamedai sasa hivi watoto watano wanalazimika kutumia kitabu kimoja hali inayosababisha washindwe kufanya mazoezi ya kazi walizopewa darasani.

Changamoto nyingine ni ukosefu wa umeme, upungufu wa madawati hali inayopunguza utulivu wa wanafunzi darasani lakini pia upungufu wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo katika shule za msingi na vyoo upande wa shule ya Sekondari Ngokolo upande wa wavulana havitoshi, ukosefu wa chumba maalum cha kujistiri katika shule ya Sekondari Ngokolo.

Kwa upande wa idadi ya walimu watoto hao wamesema hali hairidhishi mfano katika shule ya Sekondari Ngokolo kuna mwalimu mmoja pekee wa Sayansi licha ya kwamba wanafunzi ni wengi ambapo kuna mkondo A hadi H.

Wamezitaja changamoto zingine ni ukosefu wa mambomba ya maji kwenye vyoo, ukosefu wa maktaba, ukosefu wa walimu wa wanafunzi wenye mahitaji maalum, ukosefu wa vifaa vya michezo, elimu ya utengenezaji sodo pamoja na shule kutokuwa na uzio hali inayosababisha mifugo kuingia shuleni na kuharibu mimea.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Naibu Mstahiki Meya wa Manispaa amelishukuru na kulipongeza shirika la Rafiki SDO kwa kutengeneza mabaraza ya watoto na kuwajengea uwezo watoto hali inayosababisha wajiamini na kuweza kutetea haki zao.

Diwani wa Kata ya Ngokolo amesema serikali inaendelea kutatua changamoto za wananchi ikiwemo kujenga miundombinu ya shule yakiwemo madarasa na matundu ya vyoo.
Naibu Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Zamda Shaban akizungumza wakati akifungua kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kilichofanyika leo Jumamosi Mei 11,2024 katika ukumbi wa Ofisi ya Rafiki SDO Kitangili Manispaa ya Shinyanga - Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Naibu Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Zamda Shaban akizungumza wakati akifungua kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 
Naibu Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Zamda Shaban akizungumza wakati akifungua kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 
Diwani wa Kata ya Ngokolo Mhe. Victor Mkwizu akizungumza wakati wa kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 
Diwani wa Kata ya Ngokolo Mhe. Victor Mkwizu akizungumza wakati wa kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 
Meneja Mradi wa Kukuza Asasi za Kiraia (MKUA) , Maria Maduhu kutoka Shirika la Rafiki SDO akizungumza wakati wa kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 

Meneja Mradi wa Kukuza Asasi za Kiraia (MKUA) , Maria Maduhu kutoka Shirika la Rafiki SDO akizungumza wakati wa kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 
Meneja Mradi wa Kukuza Asasi za Kiraia (MKUA) , Maria Maduhu kutoka Shirika la Rafiki SDO akizungumza wakati wa kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 
Meneja Mradi wa Kukuza Asasi za Kiraia (MKUA) , Maria Maduhu kutoka Shirika la Rafiki SDO akizungumza wakati wa kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 
Wanafunzi wakiwasilisha changamoto wanazokabiliana nazo shuleni wakati wa kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 
Wanafunzi wakiwasilisha changamoto wanazokabiliana nazo shuleni wakati wa kikao cha Watoto wa Baraza la Watoto Kata ya Ngokolo na Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga 
Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata ya Ngokolo na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga  wakiwa ukumbini
Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata ya Ngokolo na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga  wakiwa ukumbini
Watoto wakifuatilia matukio ukumbini
Watoto wakifuatilia matukio ukumbini
Watoto wakifuatilia matukio ukumbini
Watoto wakifuatilia matukio ukumbini
Watoto wakifuatilia matukio ukumbini
Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata ya Ngokolo na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakifanya majadiliano
Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata ya Ngokolo na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakifanya majadiliano
Watoa Maamuzi Ngazi ya Kata ya Ngokolo na Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga wakifanya majadiliano
Mijadala ikiendelea
Mijadala ikiendelea

Mmoja wa watoto akichangia hoja wakati wa kikao hicho
Mmoja wa watoto akichangia hoja wakati wa kikao hicho
Mmoja wa watoto akichangia hoja wakati wa kikao hicho
Share:

TIGO YAKUTANA NA WADAU WAKE KWENYE JUKWAA LA WAFANYABIASHARA NA WAJASIRIAMALI SHINYANGA


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kampuni ya TIGO Tanzania imekutana na wadau wake Mkoa wa Shinyanga katika Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali lenye lengo la kutoa fursa kwa wafanyabiashara kujua huduma na bidhaa za Kibiashara, Kifedha na za dukani zilizoambatana na uboreshaji wa mtandao wa 4G+ kimkoa na Kanda ya ziwa kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa Jukwaa hilo lililofanyika Ijumaa Mei 10,2024 usiku katika ukumbi wa Karena Hotel Mjini Shinyanga, Mkurugenzi wa Kampuni ya TIGO Tanzania Kanda ya Ziwa, Joseph Mutalemwa amesema TIGO imeendelea kuboresha huduma za kuingiza sokoni bidhaa mpya hivyo kuwaomba wadau kuchangamkia fursa zinazopatikana katika Kampuni hiyo.

Amesema Kampuni  ya TIGO imetoa elimu ya bidhaa na  huduma  zake zinazorahisisha biashara kwa taasisi mbalimbali ili kuweza kukuza biashara zao na kuongeza wateja.

"Tumekutana na wadau wetu wakiwemo wafanyabiashara na wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga ili kuwaeleza na kuwatambulisha bidhaa zetu pamoja na huduma zetu zikiwemo za Mobile solutions, APN, Bulk sms, E1, Toll-free, Mjasiriamali box, 5G standalone, Collection account, Disbursement account, Huduma za kikoba, Lipa kwa Simu, Huduma simu za mkopo, Huduma za kurudisha number (simswap) na Huduma za kuoanisha number (special number)",ameeleza Mutalemwa.
Mkurugenzi wa Kampuni ya TIGO Tanzania Kanda ya Ziwa, Joseph Mutalemwa akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Kampuni ya TIGO Tanzania Kanda ya Ziwa, Joseph Mutalemwa akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga Sadock Mahundo akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga Sadock Mahundo akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga Sadock Mahundo akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Mauzo  Taasisi Ndogo na Kati wa Kampuni ya TIGO Kanda ya Ziwa, Paschal Mathew akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Mauzo Mashirika na Taasisi Kubwa wa Kampuni ya TIGO Kassongo Faraji akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Kampuni ya TIGO Tanzania Kanda ya Ziwa, Christopher Charles akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Msimamizi wa Duka Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga, Pendo Ally akieleza kuhusu Simu za mkopo zinazouzwa katika duka hilo wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Msimamizi wa Duka Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga, Pendo Ally akieleza kuhusu Simu za mkopo zinazouzwa katika duka hilo wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Msimamizi wa Duka Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga, Pendo Ally akieleza kuhusu Simu za mkopo zinazouzwa katika duka hilo wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger